SHILOH INTERNATIONAL MINISTRIES TANZANIA

Wednesday, August 13, 2014



SOMO: WATU AMBAO MBINGU ZIMEKAA KIMYA KWAAJILI YAO.
       Na:NABII FRANK JULIUS KILAWAH.

 Mbingu ni mlango au mfumo ambao Mungu anautumia kutunza na kukaa yeye mwenyewe kwaajili ya nchi. Pia tunaweza kusema Mbingu ni upeo wa Mungu katika mafundisho ya dini,ama upeo wa kiroho ambako nafsi za wafu hufikia baada ya kifo.

Mbinguni ni mahali ambapo mtakatifu Mungu wa Izrael anakaa


.
Katika kundi ambalo ninalizungumzia hapa la watu ambao mbingu zimekaa kinywa kwaajili yao.ni kundi ambalo hawatendi dhambi lakini wanahangaika kwenda kwa watumishi wa Mungu tofauti tofauti ilikupata nafasi ya kumaliza matatizo yao.jambo ambalo ni zuri lakini kwa upande mwingine sio zuri, ukienda kwa utaratibu huo utapotea lakini pia kukaa na mtumishi ambaye hamjui Mungu kwa muda mrefu itakudumaza akili yako.

Kwamaana hiyo unapo taka kukubalika ni lazima usimamie zamu yako,maana  kila mtumishi unaye muona chini ya jua amebeba maono ya Mungu kwa watu anaokubalika nao, na usipo jua wewe unataka nini na ndani mwako kumekosekana nini na niwapi utakipata, hivyo ni rahisi kusikiliza kilanayefundisha ukifikiri analo jibu la kwako.

Lakini ukijua wapi unapoelekea ili upate majibu ya matatizo yako, ukienda kwa aina hiyo utaelewa jinsi ya kuilinda roho yako lakini pia utafaniksha roho yako kukutana na unacho hitaji. 

UFUNUO 8:1.”Hata alipoifungua muhuri ya saba,kukawa kimya mbinguni kama muda wa nusu saa.Nami nikawaona wale malaika saba wasimamao mbele za Mungu,  nao wakapewa baragumu saba”.

Uwe tayari kuunganika na Mungu maana mbele yako kuna mtu ataachia nafasi kwaaji yako,maandiko yanasema muhuri wa saba ulipofunguliwa mbingu zote zikawa  kinywa, maana yake na ulimwengu wa roho ukawa kinywa kwasababu kiongozi wa ulimwengu wa roho ni mbingu na mbingu zimenyamaza kinywa kwamaana hiyo hata waombaji na wahubiri wote wapo kinywa.

Hivyo unatakiwa ujue nafasi yako ipo vipi, kwamaana huwezi kuachia vitu vingine vilivyokuwa ndani mwako ndio maana mbingu hazifunguki kwako na zimenyamaza kinywa. Pia kwaupande mwingine mbingu zinapo funga Mungu anaruhusu nafasi yaw ewe kushuka ili upate kubwa zaidi na malaika  ambao hawahitaji msaada wa mbingu wanahitaji wewe kuunganika nao ili unaposhindwa wawajibike kwako.

Unatakiwa kufaha mbinguni tunaenda kupumzika ili tuweze kwenda kwenye mbingu nyingine, hivyo mbingu inapo nyamaza nikupoteza muunganiko wa upande mmoja ilikuunganika upande mwingine,kwamaana hiyo upande wa pili ni kwaajili yako kuweza kuwajibika.

UFUNUO 9:1,2 “Malaika wa tano akapiga baragumu, nikaona nyota iliyotoka mbinguni, imeanguka juu ya nchi; naye akapewa ufunguo wa shimo la kuzimu. Akalifungua shimo la kuzimu;moshi ukapanda kutoka mle shimoni kama moshi wa tanuru kubwa;jua na anga vikatiwa giza kwasababu yaule moshi wa shimoni”.

Kwamaana hiyo mbingu haihitaji sapoti yoyote, mana mimi nimejenga ukuta mkubwa, mbingu haziwezi kufanya kitu chochote kwaajili nimesha jijengea ukuta na unanisaidia kujilinda na adui zangu.
Mwanangu kunawakati unaweza kuamka saa saba za usiku kuomba lakini mwili hautaki,usiogope,jua ni upande wa pili unakuja kwako na kupata kuunganika.elewa  mbingu zitakuwa zimenyamaza zinatafuta mafanikia ya upande wa pili kwako.

No comments: